Latest News
Posted On: May 06, 2026


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA AFYA

MAMLAKA YA DAWA NA VIFAA TIBA




ISO 9001: 2015 IMETHIBITISHWA

TAARIFA KWA WATAALAMU WA MAABARA

04 Mei, 2026

MWALIKO WA KUSHIRIKI KIKAO KUHUSU UDHIBITI WA VIFAA TIBA NA VITENDANISHI

  1. TMDA kwa kushirikiana na Chama cha Wanasayansi wa Maabara za Afya Tanzania (MeLSAT) inapenda kuwaalika wataalamu wote wa maabara kwenye kikao cha pamoja kujadili udhibiti wa vifaa tiba na vitendanishi. Kikao hiki ni muendelezo wa juhudi za Mamlaka za kuwafikia wadau wake ili kuimarisha udhibiti wa bidhaa hizo kwa nia ya kuendelea kulinda afya ya jamii.
  2. Kikao kitafanyika kwa njia ya mtandao kwa siku mbili tarehe 13 na 14 Mei, 2026 kwa kuwa na ajenda zifuatazo;
    1. Taratibu za usajili na utambuzi wa bidhaa nchini;
    2. Taratibu za ukaguzi wa maabara na maduka ya vifaa tiba na vitendanishi na Mkataba wa makubaliano (MoU) na PHLB;
    3. Utoaji wa taarifa na jinsi ya kushughulikia bidhaa za vifaa tiba na vitendanishi zisizokubalika na zisizofaa;
    4. Udhibiti wa matangazo ya vifaa tiba na vitendanishi;
    5. Uhakiki wa utendaji kazi wa vitendanishi vilivyowasilishwa nchini kwaajili ya kuomba usajili.
  3. Utaratibu na namna ya kushiriki kikao umeanishwa hapa chini: -
    Tarehe ya kikao: 13 na 14 Mei, 2026
    Muda wa kikao: Saa 7:40 mchana mpaka saa 10:00 jioni
    Kiunganishi cha kikao (link):):(Meeting ID: 882 8747 8510, Passcode: 769666)
    https://us06web.zoom.us/j/88287478510?pwd=pqsc275bmrqYuXw7G5VJi6RdcRPR9v.1
  4. Wataalamu wote wa maabara mnaombwa kushiriki kikamilifu katika kikao hiki ili kujadili changamoto zinazojitokeza wakati wa utekelezaji wa majukumu yenu ya kila siku ikiwa ni pamoja na kuweka mikakati thabiti ya kuhakikisha usalama wa afya ya wananchi.
  5. Tafadhali thibitisha ushiriki wako kwa kutuma barua pepe kupitia: octavian.aron@tmda.go.tz au namba ya simu: 0752349590.
  6. Tunatanguliza shukrani kwa ushirikiano wako.
Imetolewa Na:
Mkurugenzi Mkuu,
Mamlaka ya Dawa na Vifaa tiba (TMDA),
Kitalu Na. 56/1, Block E, Kisasa B Centre, Barabara ya Hombolo, S. L. P 1253, Dodoma au
S. L. P 77150, Dar es Salaam
Simu: +255 22 2452108/2450512/2450751
Nukushi: +255 22 2450793
Simu bila malipo: 0800110084